Other News

Mafanikio ya ZURA Tokea Kuanzishwa kwake

Nembo ya ZURA

2020-10-08
MAFANIKIO YA ZURA NDANI MIAKA 10 YA DKT. SHEIN
 
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar ni Taasisi ya Serikali iliyopo chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati ambayo imeundwa kwa Sheria Na. 7 ya mwaka 2013 kwa lengo la kudhibiti Huduma za Maji na Nishati (Umeme, Mafuta na Gesi) Zanzibar.
 
Mamlaka ilianza kazi Aprili 2015 baada ya kuteuliwa Mkurugenzi Mkuu na Bodi ya Wakurugenzi lakini ilianza rasmi kazi ya kudhibiti Huduma za Maji na Nishati Zanzibar Februari 2016.
 
ZURA hulinda maslahi ya watoaji na watumiaji wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar. Mamlaka ina jukumu la kuhakikisha kwamba huduma zinazotolewa kwa watumiaji ni nafuu, salama na za uhakika na watoaji huduma hizo wanapata faida wanayostahili kutokana na uwekezaji wao.
 
Dira: Kuwa mdhibiti bora duniani na mfano wa kuigwa katika kusimamia utoaji wa huduma bora za Maji na Nishati.
 
Dhamira: Kusimamia huduma za Maji na Nishati kwa uwazi na ufanisi ili kukuza uwekezaji na kuchangia maendeleo ya kiuchumi ya Zanzibar.
 
Kazi za ZURA

Kazi za ZURA zinajumuisha;


Mamlaka ya ZURA

Ili kufanya haya, ZURA ina Mamlaka yafuatayo:-

Kuanzisha viwango kwa bidhaa na huduma zinazodhibitiwa.

Kuhakikisha kwamba wasambazaji huduma wote wanatoa huduma zinazostahiki.

Kurahisisha na kuzishauri Sekta binafsi kuwa na ushindani mzuri.

Kuhakikisha ushirikiano wa Umma pamoja na huduma za Maji na Nishati kwa jamii kwa kufuata sheria katika shughuli zao.

Kupokea, kukabili na kutatua malalamiko ya Watumiaji wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar.

Kurahisisha utatuzi wa malalamiko na migogoro ya Wateja.

Kulinda na kutunza Mazingira, Rasilimali asilia na Afya na Usalama wa Watumiaji.
 
Mafanikio
Katika Kipindi cha Miaka Mitano (5) ZURA imepata mafanikio yafuatayo kwa ujumla:-

Ujenzi wa Jengo jipya la Ofisi za ZURA

Maandalizia ya Mradi wa Bohari na Bandari ya Mafuta na Gesi Bumbini/Mangapwani.

Ujenzi wa Nyumba za Wanakijiji cha Dundua kupisha Mradi wa Bohari na Bandari ya Mafuta na Gesi Bumbwini/Mangapwani.
 
Katika Kipindi cha Miaka Mitano (5) ZURA imepata mafanikio yafuatayo katika sekta ya Mafuta:-

Kuandaa Kanuni za kudhibiti sekta ya Mafuta.

Kutoa bei elekezi za Mafuta kila mwezi.

Kuweka fomula ya uwazi katika ukokotoaji wa bei za mafuta.

Kuhakikisha mafuta yanayoingia nchini yapo katika kiwango bora.

Kuhakikisha vipimo vya mashine za kuuzia mafuta viko sahihi.

Kutoa miongozo ya kuboresha vituo vya Mafuta.

Kutoa leseni kwa wawekezaji katika sekta ya Mafuta.

Kufanya ukaguzi mara kwa mara katika vituo na bohari za Mafuta.
 
Katika Kipindi cha Miaka Mitano (5) ZURA imepata mafanikio yafuatayo katika sekta ya Gesi (LPG):-

Kuandaa Kanuni za kudhibiti sekta ya Gesi (LPG).

Kuandaa Mikutano na Wadau wa sekta ya Gesi (LPG).

Kutoa Elimu kwa Wauzaji na Watumiaji wa Gesi (LPG).

Katika Kipindi cha Miaka Mitano (5) ZURA imepata mafanikio yafuatayo katika sekta ya Umeme:-

Kuandaa Kanuni za kudhibiti sekta ya Umeme.

Kuandaa Mikutano na Wadau kujadili Gharama ya Huduma ya usambazaji wa umeme Zanzibar (Cost of service study).

Kutoa Elimu kwa Wauzaji na Watumiaji wa Umeme.
 
Katika Kipindi cha Miaka Mitano (5) ZURA imepata mafanikio yafuatayo katika sekta ya Maji:-

Kupatikana kwa Mshauri Elekezi katika Sekta ya Maji (Consultant).

Kuisaidia ZAWA kununua Mita za Maji.

Kutoa Elimu kwa Wauzaji na Watumiaji wa Maji.
Changamoto
 
ZURA katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku inakutana na changamoto zifuatazo:-

Kutokutoa au kuchukua risiti kwa wauzaji na wanunuzi wa nishati ya mafuta.

Uelewa mdogo juu ya majukumu ya ZURA kwa Taasisi zinazodhibitiwa na jamii kwa ujumla.

ZURA itaanza rasmi kudhibiti sekta ya Umeme na Maji.
 
Mikakati

ZURA imeandaa Mpango Mkakati wa miaka mitano (2017-2022). Mpango huo uliandaliwa kufuatia mchakato kamili ambao ulijumuisha wadau, Sheria ya ZURA na nyaraka nyengine muhimu za upangaji Mipango ya kitaifa kama vile Dira ya 2020, MKUZA na Manifesto ya Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi (CCM).
 
ZURA katika kukabiliana na changamoto zilizopo imejipanga kufanya yafuatayo.

Kuongeza kasi ya kujitangaza zaidi ili jamii iweze kuelewa majukumu na uwezo wa ZURA.

Kuongeza ushirikiano na wadau wa sekta za inazosimamia.

Kutayarisha Kanuni na hati nyengine za kisheria ili kusimamia sekta ya Umeme na Maji.

Kufanya Ukaguzi wa mara kwa mara kwenye Vituo na Bohari za Mafuta.

Kuanzisha mfumo wa kuweka alama katika bidhaa za Mafuta.










 

Sign-up and we will notify you when there is news from DoEM